Friday, August 26, 2011

Adebayor aenda Tottenham

Emmanuel Adebayor

Tottenham imethibitisha kumsajili mshambuliaji Emmanuel Adebayor kwa mkopo hadi mwisho wa msimu kutoka Manchester City.
Mapema wiki hii meneja wa Tottenham Harry Redknapp alithiibitisha kuwa klabu yake iko katika mazungumzo na City kuhusiana na uhamisho wa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27. 
Adebayor hakuwa kipenzi cha meneja wa Man City, Roberto Mancini mwaka jana, na hivyo kupelekwa Real Madrid kwa mkopo.
Spurs pia wamemsajili kiungo kutoka Uhispania Yago Falque kutoka Juventus ya Italia.
Spurs na City wamekuwa wakizungumza kwa muda kuhusiana na mkataba wa Adebayor, huku ikiripotiwa kuwa mshahara wake wa pauni 170,000 kwa wiki ukiwa ndio kikwazo kikubwa.
Mancini aliweka wazi kwa mshambuliaji huyo kutoka Togo, aliyejiunga na City akitokea Arsenal kuwa hana nafasi kubwa kutokana na kuwepo kwa Carlos Tevez, Sergio Aguero, Mario Balotelli na Edin Dzeko.
Mwezi April Adebayor alisema angependa kusalia Real Madrid.
Adebayor alifunga mabao mawili dhidi ya Tottenham katika robo fainali ya Klabu Bingwa Ulaya wakati timu hizo zilipokutana kwenye uwanja wa Bernabeu msimu uliopita.

Thursday, August 25, 2011

VOT FOR MT.KILIMANJARO..


MT. KILIMANJARO NOMINATED AS CANDIDATE FOR THE NEW SEVEN NATURAL WONDERS OF THE WORLD
Mount Kilimanjaro which is the highest peak in Africa and the highest free standing mountain in the world has been nominated as a candidate for the seven natural wonders of the world, in a competition organised by an organisation known as Seven Natural Wonders in which tourist attractions from all over the world are voted to nominated as The Seven Natural wonders of The World.
Tanzania will gain much publicity from being listed in the new list of Seven Natural wonders of the World and will be able to use this opportunity to promote Mt. Kilimanjaro as being in Tanzania.
Out of the 28 contestants which have made it to this stage, only two nominations are from Africa, these being Mt. Kilimanjaro (Tanzania) and Table Mountain (South Africa). There is fierce competition between the two African destinations.
Voting trends have shown that most people who are voting for Mount Kilimanjaro are those residing outside the country and that very few Tanzanian residents are voting for Mt. Kilimanjaro unlike the case for Table Mountain where large numbers of South Africans are taking participation in voting for Table Mountain.
We (TTB) would like to urge Tanzanians (in and out of Tanzania), friends and patrons worldwide to vote for Mount Kilimanjaro so that it becomes one of the New Seven Natural Wonders Of The World.
Votes are being collected at the following website: www.new7wonders.com
Note that the competition is open until November 11th, 2011.
For more information contact:
The Managing Director,
Tanzania Tourist Board,
Dar-es-salaam
Tel: 255-22-2111244/5
Email: md@tanzaniatouristboard.go.tz

AU kuchangisha pesa za janga la njaa


Viongozi wa Afrika wanakutana katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, kuchangisha pesa ili kukabiliana na mzozo wa kibinadamu unaokabili eneo la pembe ya Afrika.

Mkutano wa leo ulitarajiwa kufanyika wiki mbili zilizopita, lakini ukaahirishwa ili kuupa Muungano wa Afrika muda zaidi kuandaa mkutano huo.
Dola millioni moja na nusu zaidi zinahitajika kukabiliana na janga la njaa, linaloathiri nchi tano barani Afrika. Somalia ambako mzozo wa kisiasa bado unaendelea ndiyo iliyoathirika zaidi .
Mkutano huu wa kuchangisha fedha ni wa kwanza wa aina yake kufanywa na Muungano wa Afrika.
Mwenyekiti wa Tume ya Muungano wa Afrika, Jean Ping, amesema juhudi za muungano huo hazitoshi na madhumuni ya mkutano huu wa siku moja ni kuchangisha dola billioni moja na nusu kufadhili janga hilo.
Nchi kadhaa za Afrika tayari zimetoa michango yao katika juhudi hizo za kibinadamu, lakini muungano huo umeshutumiwa kwa kuchelewa kushughulikia janga hilo kwa haraka.
Hata hivyo, Muungano huo umejitetea na kusema ulihitaji muda zaidi kushirikiana na wanachama wake na kuandaa mkutano.
Waandalizi wa mkutano huu wanasema mkutano wenyewe hautachangisha pesa pekee , lakini pia viongozi watajadili suluhu za kudumu za kukabiliana na majanga ya kibinadamu barani Afrika.

VICTOR COSTA AREJESHWA STARS....!

 
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen leo (Agosti 25 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya mechi ya mchujo dhidi ya Algeria ‘Desert Warriors’ kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon.
Wachezaji walioitwa ni makipa Shabani Dihile (JKT Ruvu Stars), Juma Kaseja (Simba) na Shabani Kado (Yanga). Mabeki wa pembeni ni nahodha Shadrack Nsajigwa (Yanga), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya) na Amir Maftah (Simba). Mabeki wa kati ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba) na Victor Costa (Simba).

Viungo wakabaji ni Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Juma Seif (Yanga) na Jabir Aziz (Azam). Viungo washambuliaji ni Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam) na Salum Machaku (Simba).

Washambuliaji ni Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Ramadhan Chombo (Azam), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden) na John Bocco (Azam).

Timu itaingia kambini Jumapili (Agosti 28 mwaka huu) mchana na jioni itaanza mazoezi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. Mechi dhidi ya Algeria itachezwa Septemba 3 mwaka huu kuanzia saa 10.00 jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wenger asifu moyo wa vijana


Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amewasifu vijana wake kwa kumuondolea mashaka na wasiwasi uliotanda na kuikumba klabu hiyo katika majuma ya hivi karibuni kwa kuiondoa klabu ya Utaliano Udinese na hivyo kujipatia tiketi ya kushiriki michuano ya hatua za Ligi ya mabingwa.