Thursday, December 29, 2011

TAMKO LA CHADEMA KWA SERIKALI YA ISRAEL.....!

Serikali itake Israel waombe radhi; tukijiheshimu, tutaheshimiwa
Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa ya CHADEMA inaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa tamko juu ya kauli ya Waziri wa Ulinzi wa Israel ya kwamba nchi yetu si ya muhimu wala ya maana.
Waziri Barak alifanya mahojiano na Radio Israel na kutoa kauli ambayo imenukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari vya nchi hiyo wiki iliyopita kuwa “ Germany, France and England are not Tanzania, Mauritania or Tripolitania…..these are very important, very relevant countries and we don’t have an interest in increasing tensions with them or making them bitter enemies”.
Kwa kauli hii serikali ya Israel inaiona Tanzania sio nchi ya muhimu wala ya maana hata kufikia hatua ya kuilinganisha na eneo tu ndani ya Libya linaloitwa Tripolitania.
Tunamtaka Waziri wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa, Benard Membe kuitaka serikali ya Israel kuomba radhi kufuatia kauli hiyo au kueleza wazi iwapo mazungumzo hayo ya Waziri Barak ni msimamo wa nchi hiyo kuhusu uhusiano wa kidiplomasia wa mataifa yetu.

                     Huyu ndiye Ehud-Barak waziri wa Urinzi wa Israel


Barua pekee ya balozi wa heshima wa Tanzania nchini Israel, Kasbian Nuriel Chirich kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Avigdor Lieberman ya kulaani matamshi hayo ya Waziri Barak na kumkaribisha mwakilishi wa Israel kutembelea Tanzania haitoshi kuifanya serikali ya nchi hiyo kutambua athari za kidiplomasia za kauli iliyotolewa.


Aidha kwa kuwa serikali imekuwa ikieleza kwamba Tanzania ina mahusiano mazuri ya kiulinzi na Israel, ni muhimu pia Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dr Hussein Mwinyi akaeleza umma iwapo kauli hiyo ya Waziri Barak ndio msingi wa mahusiano yaliyopo kati ya nchi zetu kuhusu ulinzi na usalama.

Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa inachukua fursa hii kurudia kuwakumbusha watanzania kwamba kupuuzwa huku kwa nchi yetu katika medani ya kimataifa kunatokana na sera mbovu ya mambo ya nje chini ya utawala wa sasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).



Tanzania imepoteza heshima katika siasa za dunia kutokana na diplomasia yetu kujikita katika kuomba omba kimataifa; pamoja na kuwa kimaneno na maandishi serikali inazungumza kuhusu diplomasia ya kiuchumi, kivitendo mahusiano yetu yamejengeka katika misingi ya utegemezi, kupungua kwa urari wa kibiashara na kuachia mianya ya uporwaji wa rasilimali.


Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa inatambua kwamba wakati wa uongozi wa awamu ya kwanza wa hayati Mwalimu Julius Nyerere, Tanzania ilikuwa na heshima na sauti kimataifa sio tu katika jitihada za ukombozi kusini mwa Afrika bali pia katika mahusiano ya kisiasa, kiuchumi na kijamii baina ya nchi za kusini na mataifa mengine duniani.


Hali ya Tanzania kupoteza sauti katika medani ya kimataifa imedhihirika pia hivi karibuni katika mkutano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi (COP 17) uliomalizika hivi karibuni nchini Afrika Kusini; wakati nchi yetu ikiwa ni miongoni mwa waathirika wakubwa zaidi wa mabadiliko ya tabia nchi. Iwapo hatua hazitachukuliwa kurejesha heshima na sauti ya Tanzania kimataifa maamuzi mengi yatafanyika yenye athari kwa wananchi wengi bila ushiriki wao thabiti kama yanayoendelea hivi sasa kuhusu Mikataba ya Kiuchumi na Nchi za Jumuia ya Ulaya (EPA) yenye madhara kwa wakulima na wenye viwanda nchini.

Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa inatoa mwito kwa watanzania kuendelea kuunganisha nguvu ya umma kusimamia uwajibikaji na kufanya mabadiliko ya kimsingi ya kiuongozi, kisera na kimfumo ya kitaifa ili kuweza kurejesha nafasi na heshima ya Tanzania kimataifa katika mazingira ya sasa ya ushindani wa kiuchumi, kiulinzi, kijamii na kisiasa.

Kauli ya Waziri Barak nimuendelezo tu wa mataifa mbalimbali kuifanya Tanzania na baadhi ya nchi nyingine za Afrika kuwa hazina heshima wala sauti katika siasa za kimataifa kama ambavyo Serikali za Uingereza na Marekani zimeweka masharti yenye mwelekeo wa ukoloni mamboleo kuhusu masuala ya ushoga na usagaji.


Hatua za kupinga kauli za kudharauliwa na kulazimishwa mambo tusiyoyataka ziende sambamba na kudhibiti mianya yote ya ufisadi wa kimataifa, uwekezaji uchwara na kutetereka kwa misingi wa utawala wa kisheria masuala ambayo yanasababisha migogoro na pia rasilimali za nchi kutokutumika kwa manufaa ya wananchi walio wengi; tukijiheshimu, tutaheshimiwa.


Wenu katika Demokrasia na Maendeleo,

John Mnyika (Mb)



Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa (CHADEMA)

Wednesday, December 14, 2011

MOVIE: MKWAWA SHUJAA WA MASHUJAA – IN STORES 10.12.2011

Mkwawa was the chief of Uhehe who won fame by defeating Germans at Lugalo on 17th August 1891 and maintaining their resistance for seven years until he shot himself to death. Mkwawa is derived from Mukwava short form of Mukwavinyika, meaning the conqueror of many lands. He was born at Luhota in 1855.

Uhehe occupies the Iringa region of southern Tanzania in East Africa, its citizens (Hehe) are Bantu speaking people.

The history of Chief Mkwawa has always fascinated me since I was a little kid. After I acquired enough IT skills, the idea of putting the history on the web was always lingering in my mind. The only obstacle was that, the Internet technology in Tanzania was not that much developed and hence hampered my effort.

After having exposed to the world of IT, my effort was rekindled and revived. The first biggest step I did was to register the domain mkwawa.com. However another obstacle came, I did not have any authentic and reliable source of information.
Fortunately a freelance filmmaker in Germany, Mr. Martin Baer, eventually bumped into my personal web page http://www.mkwawa.com/immkwawa while searching for any of Chief Mkwawa’s descendants on the Internet. He too was interested with Chief Mkwawa’s history and had a plan to make a documentary film since 1996. Martin managed to secure funds for the project and chose me to be the main actor. I took that opportunity to collect relevant materials of Chief Mkwawa’s history while filming in both Tanzania and German.

I am really grateful with what I had collected from interviewing people, reading history books and visiting historic places.This is an account of my itinerary. Hopefully you will find this site enjoyable as well as informative.

Friday, December 2, 2011

KOCHA WA SIMBA AWAUZA OKWI NA KAZIMOTO ULAYA....

Milovan Cirkovic ‘Profesa Chico’.

KOCHA Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic ‘Profesa Chico’, amesema wachezaji wake wawili, kiungo Mwinyi Kazimoto na Emmanuel Okwi, wana nafasi ya kucheza soka barani Ulaya.
Prof Chico alimshuhudia Kazimoto katika mechi dhidi ya Djibouti lakini akalazimika kumsaka Okwi kwenye mtandao baada ya kusikia amefunga mabao matatu katika mechi moja ‘hat-trick’.
                                                   Mwinyi Kazimoto

                                                  Emmanuel Okwi

“Baada ya kumuona Okwi, nimefurahi sana kugundua ana kiwango kizuri kama nilivyokuwa nikielezwa. Najua kila kitu nitapanga nitakapokutana nao na kuanza kazi lakini ni wachezaji wanaoweza kucheza Ulaya.

“Ninaamini Simba ina wachezaji wengi wa aina hiyo, bado naendelea kuwaangalia wengine na nitaenda kuangalia mechi karibu zote za Kombe la Chalenji kwa ajili ya kuona wachezaji wangu, wa timu pinzani na wengine,” alisema Prof Chico, raia wa Serbia, aliyechukua nafasi ya Mganda, Moses Basena.

Kazimoto alionyesha kiwango cha juu katika mechi kati ya Kilimanjaro Stars dhidi ya Djibouti ikiwa ni pamoja na kufunga bao safi katika ushindi wa mabao 3-0.

Mserbia huyo amesisitiza, anataka kuona kikosi chake kinacheza mpira wa kuvutia kabla ya kuanza kusaka mabao.
“Mkicheza pasi za uhakika ni rahisi kutimiza malengo. Angalia wanavyofanya Barcelona au hata Arsenal, nataka tucheze vile,” alisema Mserbia huyo.