Wednesday, July 6, 2011

SIMBA YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME…!!!

Wachezaji wa timu ya Simba wakishangilia baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Bunamwaya ya Uganda katika mchezo wa Robo Fainali Kombe la Kagame uliochezwa Julai 5,2011 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, sasa Simba imetangulia katika fainali hizo ambapo itamenyana na El Mereikh ya Sudan katika mechi ya nusu fainali mwishoni mwa wiki, ambapo El Mereikh ilikata tiketi hiyo baada kuifunga Ulinzi ya Kenya katika mchezo uliomalizika Julai 5,2011 kwa njia ya matuta.(Kwa hisani ya Blog ya Dina Ismail).

1 comment: